*Asisitiza kwamba kazi ndiyo msingi wa maendeleoWAZIRI
MKUU Kassim Majaliwa amewataka vijana wafanye kazi kwa bidii na maarifa
kwa sababu kazi ndiyo msingi wa maendeleo yao na Taifa kwa ujumla.Pia
amewasihi wananchi wanaoishi katika maeneo ya mipakani wahakikishe
suala la kulinda mipaka hiyo linapewa kipaumbele ili kuimarisha amani na
utulivu nchini.Waziri Mkuu ametoa kauli hiyo
leo (Jumamosi, Machi 24, 2018) wakati akizungumza na wananchi
alipowasili katika uwanja wa ndege wa Nachingwea.Waziri
Mkuu ambaye yuko wilayani Ruangwa kwa ziara ya kikazi ya siku mbili
amesema ili vijana waweze kupata maendeleo lazima wafanye kazi kwa
bidii.Pia Waziri Mkuu ametumia fursa hiyo
kuwakumbusha wananchi wanaoishi katika maeneo ya mipakani washirikiane
na Serikali katika kuimarisha ulinzi na usalama.Katika
hatua nyingine, Waziri Mkuu amekagua ukarabati wa kituo cha afya cha
Kata ya Mbekenyera na kuwaeleza wananchi dhamira ya Serikali ya
kuwahudumia.Amesema Serikali imetoa sh.
milioni 500 kwa ajili ya ujenzi wa wodi ya kujifungulia, maabara, wodi
ya wanawake na wanaume na chumba cha upasuaji.“Serikali
imeamua kuimarisha sekta ya afya kwa kujenga na kuboresha vituo vya
afya ili kuhakikisha wananchi wanapata huduma za afya karibu na makazi
yao.”Aidha, Waziri Mkuu amewataka wananchi
hao waendelee kuiunga mkono Serikali yao, ambayo imedhamiria kuwatumikia
ili waweze kupata maendeleo.Pia, Waziri Mkuu
amekabidhi gari la kubeba wagonjwa katika kituo hicho. Gari hilo
limetolewa na Rais Dkt. John Magufuli ili kuimarisha huduma za afya
kituoni hapo.IMETOLEWA NA:OFISI YA WAZIRI MKUU,JUMAMOSI, MACHI 24, 2018.
Mkurugenzi
Mtendaji wa Kampuni ya Bia ya Serengeti (SBL) Helene Weesie, jana
alifanya mazungumzo na maofisa kutoka Wizara ya Mambo ya Ndani ikiwa ni
sehemu ya uboreshaji zaidi wa maslahi na mazingira ya kazi kwa
wafanyakazi wa kampuni hiyo. “Tukiwa kama kampuni inayoheshimu sheria
na kujali maslahi ya wafanyakazi wetu na nchi kwa ujumla, tumekuwa
tukikutana na mamlaka husika ili kuhakikisha haki na maslahi ya
wafanyakazi wetu yanalindwa na kuheshimiwa.,” anasema Weesie SBL
imeajiri wafanyakazi zaidi ya 700 katika viwanda vyake vilivyopo Moshi,
Mwanza na Dar es Salaam. Bia yake mama ya Serengeti Premium Lager
ilizalishwa kwa mara ya kwanza kwa kutumia kimea kwa aslimia 100 na
imeweza kushinda zaidi ya tuzo kumi za dhahabu za kitaifa na kimataifa.Tangu
kuanzishwa kwake mwaka 2002, SBL imekuwa huku ikiongeza idadi ya
bidhaa inazozalisha. Baada ya kisisi iikubwa cha hisa kuchukuliwa na
Kampuni ya Bia ya AFRIKA Mashariki (EABL)/Diageo mwaka 2010 kumekuwepo
uwekezaji mkubwa amboa umefanikisha uzalishaji w3a bidhaa zenye ubora
wa kimataifa na kutengeza fursa kwa Watanzania.Moja
kati ya nguzo za Diageo ambayo ni kampuni mama YA sbl ni kujenga na
kuwawezesha wafanyakazi wake sehemu yoyote inapofanya kazi ikiwamo
Tanzania. Kutokana na hili idadi ya wataalamu wageni imepungua kwa kiasi
kikubwa kutoka zaidi ya 30 hadi sita kufikia mwezi Machi 2018 ikiwa ni
chini ya asilimia 1 ya nguvu kazi katika kampuni“Tunapenda
kuwahakikishia wateja wetu kuwa tutaendelea kuimarisha mahusiano na
wafanyakazi wetu. Tutaendelea kukidhi mahitaji yao kwa kuwahakikishia
bidhaa bora ikiwa ni sehemu muhimu kwa biashara yetu,”anasema mkurugenzi
huyo.Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Bia ya Serengeti (SBL) Helene Weesie,
Mbunge
wa Mtama (CCM), Nape Nnauye amezungumzia tukio la kutishiwa bastola
wakati akitaka kuzungumza na waandishi wa habari nje ya Hoteli ya Protea
lililotokea baada ya kuachwa katika mabadiliko madogo ya Baraza la
Mawaziri.Katika ukurasa wake wa mtandao wa kijamii wa Twitter, Nape amekumbushia tukio hilo la Machi 23, 2017 na kuandika,
“mwaka mmoja uliopita tarehe kama ya leo Mwenyezi Mungu aliniokoa na
mdomo wa bunduki wa wanyama wasiopenda haki! Mungu mkubwa, mbegu ya haki
haifi.”Katika
ujumbe huo Nape aliweka picha yake ya video akizungumza na waandishi wa
habari nje ya hoteli hiyo kueleza masuala mbalimbali, huku akiwataka
vijana kudai haki zao bila woga.Mtu
aliyemtishia bastola Nape alikuwa pamoja na wenzake wawili ambao kwa
pamoja walikuwa wakimlazimisha arudi kwenye gari lake na kuondoka,
lakini mbunge huyo aligoma na ndipo (mtu huyo) aliporudi nyuma na
kuchomoa bastola kutoka kiunoni kisha kumtishia kabla ya kutulizwa na
mwezake.Baada ya tukio hilo watu hao walitoweka eneo hilo muda mfupi baadaye.Kufuatia
tukio hilo Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mwigulu Nchemba alisema
mtu aliyemtishia bastola Waziri huyo wa zamani wa Habari, Utamaduni,
Sanaa na Michezo hakuwa askari wa Jeshi la Polisi.Soma: Mwigulu: Aliyemtishia Nape bastola si polisiMwigulu
alieleza hayo baada ya kufungua mkutano wa kazi wa mwaka wa maofisa
waandamizi wa polisi, makamanda wa mikoa na wakuu wa vikosi wa Jeshi la
Polisi uliofanyika mjini Dodoma.Hata hivyo, Mwigulu alikataa kueleza kwa undani kuhusu mtu huyo kwa kubainisha anatoka taasisi gani wala jina lake.
Mwaka
mmoja uliopita tarehe kama ya leo Mwemyezi Mungu aliniokoa na mdomo wa
bunduki wa wanyama wasiopenda haki! Mungu mkubwa, mbegu ya haki haifi! pic.twitter.com/M6PqupQQWK— Nape Moses Nnauye (@Nnauye_Nape) March 23, 2018
Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Manendeleo (CHADEMA), Freeman
Mbowe amefunguka na kuonyesha wasiwasi juu ya Jeshi la polisi kutaka
kuwabambikizia kesi za mauaji au uhaini ili waweze kuwekwa mahabusu muda
mrefu.
Mbowe amesema hayo leo Machi 22, 2018 ikiwa ni siku ambayo yeye pamoja
na viongozi wengine wa chama hicho wanatakiwa kufika katika kituo cha
polisi kusikiliza wito wa jeshi hilo na kusema kuwa wamepata taarifa
zingine kuwa Mbunge wa Iringa Mjini Mchungaji Peter Msigwa anataka
kuhusishwa katika shauri hilo ambalo wao wanalo.
"Tuna taarifa pia ya kusudio la kumuunganisha Mhe. Peter Msigwa, Mb,
Mwenyekiti wa CHADEMA Kanda ya Nyasa (Rukwa, Songwe, Mbeya, Njombe na
Iringa) na Mjumbe wa Kamati Kuu katika shauri hili. Lakini pia katika
wakati nenda rudi hii ikiendelea, tuna taarifa (asante teknolojia) kuwa
zinapangwa njama mahususi za kutubambikia viongozi wa Chadema kesi za
mauaji au Uhaini ili kuhalalisha azma ya Watawala kutuweka mahabusu kwa
muda mrefu, wakidhani kwa kufanya hivyo watakuwa wamefanikisha kufifisha
na hata kuua kabisa uwepo wa Upinzani katika Taifa" alisema Mbowe
Leo Machi 22, 2018, mimi Mwenyekiti wa CHADEMA Freeman Mbowe na
viongozi wengine waandamizi wa CHADEMA akiwepo Mhe Vincent Mashinji
(Katibu Mkuu), Mhe. John John Mnyika, Mb na Naibu Katibu Mkuu Bara, Mhe.
Salum Mwalimu, Naibu Katibu Mkuu, Zanzibar; Mhe Halima J.Mdee, Mb,
Mwenyekiti wa Bawacha, Taifa na Mjumbe wa Kamati Kuu, Mhe.John W. Heche,
Mb, Mwenyekiti wa Chadema Kanda ya Serengeti (Mara, Simiyu na
Shinyanga) na Mjumbe wa Kamati Kuu; Mhe. Esther N. Matiko, Mb,
Mwenyekiti wa Bawacha Mkoa wa Mara na Mweka hazina wa Bawacha Taifa
wanatakiwa kufika Makao Makuu ya jeshi la polisi kwa mahojiano.
Fursa 150 za Biashara na Miradi Mbalimbali Nchini Tanzania
1. Kununua Mashine za kukoroga zege na kukodisha. 2. Kununua Mashine za kukata vyuma na kuzikodisha. 3. Kutengeneza na kuuza tofali 4. Ufundi, Website updating/Database: Katika Halmashauri, Manispaa, Mashule, Wizara, Wilaya na Makampuni mbalimbali. 5. Kuanzisha kituo cha redio na televisheni 6.
Kufunga na kutengeneza vifaa mbalimbali vya electroniki na mawasiliano
mfano; compyuta na vifaa vya compyuta na mawasiliano. 7. Kuuza software; mfano Antivirus, Operating Systems, Pastel, Tally, Myob, n.k 8. Kushona na kuuza nguo. 9. Kufungua Duka la kuuza nguo mpya; suit, socks, batiki, nguo za asili, Mashuka, Mashati, Suruali, 10. Ufugaji wa mifugo mbalimbali mfano Kondoo, Mbuzi, Ng’ombe, Kuku, Bata, na wengine. 11. Kufungua stationery, kuuza (supply) vitabu na vifaa mbalimbali ktk mashule na vyuo. 12. Kutoa ushauri mbalimbali wa Kitaalamu. 13. Kuuza viazi, mahindi, mihogo, kutengeneza popcorn na kuziuza. 14. Kusajili namba za simu na kuuza vocha 15. Kuwa na mradi wa Pikipiki zisizotumia mafuta na zinazotumia mafuta 16. Kilimo cha mazao mbalimbali kulingana na hali ya hewa ya sehemu husika. 17. Kuuza Mitumba 18. Kusimamia miradi mbalimbali 19. Kufungua duka la kuuza mitambo mbalimbali 20. Kufungua banda la chakula na chips 21. Kukodisha turubai viti na meza 22. Kufungua Supermarket 23. Kufungua Saluni 24. Kufungua Bucha 25. Video Shooting & Editing. 26. Kufungua Internet cafe 27. Duka la kuuza matunda 28. Kufungua duka la kuuza vifaa vya simu za mkononi na landline. 29. Kufungua duka la vifaa vya ujenzi; cement, vifaa vya umeme, duka la mabati 30. Kutengeneza michoro mbalimbali ya majumba na miradi ya ICT 31. Kuchapa vitabu, bronchures, n.k 32. Kuanzisha kampuni ya ujenzi (Building contractor) 33. Kuuza Vifaa vya umeme wa nishati ya jua (solar) ,battery, inverter na vifaa vingine vya solar n.k 34. Kuuza maji kwa jumla na rejaleja. 35. Kutengeneza na kuuza Unga wa lishe bora. 36. Kukodisha Music 37. Kuanzisha Mradi wa Taxi 38. Kuanzisha mradi wa Daladala 39. Kuuza vifaa vya Kompyuta, laptops, converters, HDDs, Monitors, Softwares, CD Copiers na vifaa vingine. 40. Kununua magenerator na kukodisha 41. Kufungua kampuni ya kutoa huduma za simu 42. Kufungua kampuni ya kutoa huduma za internet (ISP) 43. Kuuza mabati na vigae 44. Kujenga apartments 45. Kufungua Kisima cha mafuta ya taa au mafuta ya aina zote 46. Kufungua Duka la samaki 47. Kufungua Duka la nafaka 48. Kufungua Shule za Awali, Shule za Msingi, Sekondari na Vyuo. 49. Kujenga hostel 50. Kuuza vocha na ving’amuzi vya DStv, Zuku, Startimes, Easy TV, TNG, Digitech, Continental. 51. Kujenga mtambo wa kuzalisha umeme na kuuza katika viwanda na wananchi. 52. Ufundi simu 53. Kufungua Hospitali, Zahanati. 54. Maabara ya Macho, Meno 55. Kuchimba/Kuuza Madini 56. Kufungua ofisi ya kutoa huduma ya simu na fax 57. Kuuza miti na mbao 58. Kufungua Grocery, bar 59. Kufungua studio ya kupiga na kusafisha picha 60. Kucharge simu/battery 61. Duka la TV na vifaa vingine 62. Kuanzisha biashara ya kuuza vyakula katika sherehe na tamasha mbalimbali (catering). 63. Banda la kupigisha simu 64. Kuuza na kushona Uniform za shule 65. Kuanzisha duka la kuuza vitu kwa jumla. 66. Kufungua gereji za kutengeneza bajaji, pikipiki na magari 67. Kuuza vyuma, pembejeo, rake, jembe 68. Kuuza fanicha 69. Kufungua sehemu ya kuziba pancha za matairi ya magari na mitambo. 70. Kujenga nyumba za kulala wageni (hotel) 71. Kuagiza na kuuza vifaa vya aluminium. 72. Kuuza vioo 73. Kushona na kukodisha nguo za harusi 74. Kufungua yard kwa ajili ya kuosha magari 75. Kuuza mashine za kuchomelea (welding machine). 76. Kuuza vifaa vya kuvaa Site (boots, helmets etc) 77. Kununua mabasi kwa ajili ya kusafirisha wanafunzi 78. Kufungua studio ya kutengeneza vipindi vya redio na televisheni 79. Kuanzisha ofisi ya michezo ya televisheni (TV Games) 80. Kufungua benki 81. Kuwa na malori ya kubeba kokoto na mchanga 82. Kuuza vifaa mfano TV, CCTV Camera, n.k 83. Kuwa dalali wa vitu mbalimbali 84. Kuanzisha mradi wa kukodisha fork lift na winchi (crane) 85. Kuanzisha kiwanda cha kutengeneza viatu. 86. Kuanzisha viwanda mbalimbali 87.
Duka la vifaa vya simu na gadgets mbalimbali zinazoendana na
mawasiliano ya Vodacom, TTCL, AIRTEL, TIGO, ZANTEL, n.k. 88. Kujenga Ukumbi wa kukodisha kwa sherehe, mikutano mbalimbali 89. Kununua matrekta, mitambo ya ujenzi wa barabara na kukodisha 90. Kutengeneza antenna na kuuza 91. Kufungua mradi wa Machine za kusafisha, kutoboa na kuchana mbao 92. Kufungua mradi wa kuuza vifaa vya Umeme wa kutumia upepo 93. Biashara ya kuagiza magari 94. Kufanya biashara za Jukebox 95. Kukodisha matenki ya maji 96. Kufungua duka la kuuza Asali 97. Kutengeneza Mikokoteni/ matoroli na kuikodisha 98. Kufungua Duka la vinyago, batiki 99. Kuanzisha huduma ya AIRTEL MONEY, MPESA, TIGOPESA, EZY PESA 100. Kuanzisha sehemu ya kufanyia mazoezi (Gym). 101. Kununua na kuuza vifaa vya kupima ardhi. 102. Kufungua duka la kuuza dawa (pharmacy). 103. Kufungua Kampuni ya Ulinzi 104. Kufungua kampuni ya "Clearing and fowarding" 105. Kuchezesha vikaragosi 106. Kuuza spea za bajaji, magari na pikipiki 107. Kuuza baiskeli 108. Kuuza magodoro 109. Kuuza vyombo mbalimbali kwa ajili ya matumizi ya nyumbani mfano bakuli, sahani, vikombe, vijiko, 110. Kuuza marumaru (limestones) 111. Kuuza kokoto 112. Kuuza mchanga 113. Kufundisha Tuisheni 114. Biashara za bima 115. Kampuni ya kusafirisha abiria kwa njia ya anga (ndege) 116. Biashara za kitalii 117. Biashara za meli na maboti. 118. Kampuni ya kuchimba visima 119. Kufungua ofisi ya wakili/mawakili wa kujitegemea 120. Kuuza mkaa 121. Kutengeneza mashine za kutengeneza tofali 122. Kampuni ya kupima ardhi 123. Kampuni ya magazeti 124. Kuchapa (printing) magazeti 125. Kuuza magazeti 126. Kuchimba mafuta 127. Kiwanda cha kutengeneza mabati 128. Kiwanda cha kutengeneza fanicha 129. Kiwanda cha kutengeneza matairi 130. Kutengeneza vitanda vya chuma 131. Kununua nyumba katika Maghorofa (Apartments) na kuzikodisha. 132. Kukodisha makapeti 133. Kupamba maharusi na kumbi za harusi/sherehe. 134. Mashine ya kusaga na kukoboa nafaka. 135. Kazi ya ususi na kusafisha kucha. 136. Kuuza Gypsum 137. Malori ya kubeba mafuta na Mizigo 138. Duka la kuuza mboga za majani 139. Duka la kuuza maua. 140. Kampuni ya kuzoa takataka 141. Kampuni ya kuuza magari 142. Kuuza viwanja 143. Uvuvi 144. Kutengeneza na kuuza nguzo za kujengea fensi 145. Uchoraji wa mabango. 146. Duka la kuuza silaha 147. Ukumbi wa kuonesha mpira 148. Biashara ya mlm (network marketing) 149. Yadi kwa ajili ya kupaki magari 150. Mradi wa trekta za kukodisha kwa ajili ya kilimo
Mtu mmoja aliyefahamika kwa jina la AHADI MGAYA
mwenye umri kati ya 30-33 mkazi wa mtaa wa mwafute kata ya ilemi mkoani mbeya
ameaga dunia baada ya kujinyonga usiku wa kuamkia leo.
Akiongea barozi wa mtaa
wa mwafute JAPHETI MAHINYAamesema kuwa
yeye alipewa taarifa ya marehemu kutoweka nyumbani jana kupitia mke wake na
marehemu kusema kuwa mpaka sasa chanzo cha tukio hilo hakijafahamika kwani
hakuwa na mgogoro wowote.
Hata hivyo MAHINYA
ametoa wito kwa wananchi kutojichukulia sheria mkononi na badala yake kama
kutakuwa na tatizo au mgogoro wowote ni heri kushaulisha watu wanaokuzunguka
kabla ya kuchukua hatua yoyote.
Nao majirani wa
marehemu FRANCIS TAMIMU pamoja na SOPHIA wameeleza kupokea kwa mshituko tukio
hilo na kutoa wito kwa wananchi wengine kutokuchukua hatua za kujinyonga kwa
hupelekea maumivu makali kwa familia na jamii inayomzunguka.
Kwa upande wake kamanda
wa jeshi la polisi mkoa wa mbeya MHAMED MPINGA amethibitisha kutokea kwa tukio
hilo na kutoa wito kwa wananchi kutokatisha maisha yao kwa namna yoyote ile
kwani huacha majonzi na simanzi kwa wanafamilia.
Wananchi wa
mtaa wa mapambano kata ya iyela wametakiwa kuchangia ujenzi wa vyoo unaoendelea
katika shule ya msingi mapambano ili kufanya mwendelezo wa sehemu alipoishia
mdau aliyekuwa akijenga vyoo hivyo ndele mwaselela.
Hayo yameelezwa na afisa mtendaji wa mtaa wa mapambano katika
kata ya iyela kizito nenalo katika mkutano wa wazazi uliofanyika katika viwanja
vya shule ya msingi mapambano uliofanyika mapema hii leo.
Nenalo amesema wananchi hawanabudi kutambua kuwa afya ya
mtoto inawahusu wote na hivyo wanapaswa kutoa mchango huo wa shilingi elfu tatu
ili kuhakikisha kuwa ujenzi huo unakamilika.pia amewapongeza baadhi ya wananchi
ambao wameonesha mwitikio mzuri katika suala hilo.
Mwenyekiti wa mtaa wa mapambano mwinjilisiti mwampetele
amesema kuwa wananchi wanatakiwa kujitoa kwa vitendo na siyo maneno ikiwa ni
pamoja na kuhudhuria mikutano inayoitishwa kwa lengo la kujua maendeleo ya mtaa
wao.
Kwa upande wake joji mwangonele ambaye ni mwenyekiti wa
kamati ya shule ya msingi mapambano amesema kuwa wazazi hawanabudi kutilia
mkazo katika kufuatilia maendeleo ya watoto wao ili kuhakikisha yanakuwa
mazuri.
Nao baadhi ya wazazi waliohudhuria mkutano huo Richard
salingo pamoja na anastazi mwampashe wameeleza kuwa suala hilo wamelipokea
vizuri na kuwataka wale ambao bado wanasitasita katika masula haya ya maendeleo
kutokufanya hivyo.