Jumamosi, 24 Machi 2018

Mbowe afunguka kumhofia Mbunge Msigwa

Mbowe afunguka kumhofia Mbunge Msigwa


Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Manendeleo (CHADEMA), Freeman Mbowe amefunguka na kuonyesha wasiwasi juu ya Jeshi la polisi kutaka kuwabambikizia kesi za mauaji au uhaini ili waweze kuwekwa mahabusu muda mrefu.

Mbowe amesema hayo leo Machi 22, 2018 ikiwa ni siku ambayo yeye pamoja na viongozi wengine wa chama hicho wanatakiwa kufika katika kituo cha polisi kusikiliza wito wa jeshi hilo na kusema kuwa wamepata taarifa zingine kuwa Mbunge wa Iringa Mjini Mchungaji Peter Msigwa anataka kuhusishwa katika shauri hilo ambalo wao wanalo.

"Tuna taarifa pia ya kusudio la kumuunganisha Mhe. Peter Msigwa, Mb, Mwenyekiti wa CHADEMA Kanda ya Nyasa (Rukwa, Songwe, Mbeya, Njombe na Iringa) na Mjumbe wa Kamati Kuu katika shauri hili. Lakini pia katika wakati nenda rudi hii ikiendelea, tuna taarifa (asante teknolojia) kuwa zinapangwa njama mahususi za kutubambikia viongozi wa Chadema kesi za mauaji au Uhaini ili kuhalalisha azma ya Watawala kutuweka mahabusu kwa muda mrefu, wakidhani kwa kufanya hivyo watakuwa wamefanikisha kufifisha na hata kuua kabisa uwepo wa Upinzani katika Taifa" alisema Mbowe

Leo Machi 22,  2018, mimi  Mwenyekiti wa CHADEMA Freeman Mbowe na viongozi wengine waandamizi wa CHADEMA akiwepo Mhe Vincent Mashinji (Katibu Mkuu), Mhe. John John Mnyika, Mb na Naibu Katibu Mkuu Bara, Mhe. Salum Mwalimu, Naibu Katibu Mkuu, Zanzibar; Mhe Halima J.Mdee, Mb, Mwenyekiti wa Bawacha, Taifa na Mjumbe wa Kamati Kuu, Mhe.John W. Heche, Mb, Mwenyekiti wa Chadema Kanda ya Serengeti (Mara, Simiyu na Shinyanga) na Mjumbe wa Kamati Kuu; Mhe. Esther N. Matiko, Mb, Mwenyekiti wa Bawacha Mkoa wa Mara na Mweka hazina wa Bawacha Taifa wanatakiwa kufika Makao Makuu ya jeshi la polisi kwa mahojiano.

FURSA 150 ZA BIASHARA TANZANIA

Fursa 150 za Biashara na Miradi Mbalimbali Nchini Tanzania

1. Kununua Mashine za kukoroga zege na kukodisha.
2. Kununua Mashine za kukata vyuma na kuzikodisha.
3. Kutengeneza na kuuza tofali
4. Ufundi, Website updating/Database: Katika Halmashauri, Manispaa, Mashule, Wizara, Wilaya na           Makampuni mbalimbali.
5.  Kuanzisha kituo cha redio na televisheni
6. Kufunga na kutengeneza vifaa mbalimbali vya electroniki na mawasiliano mfano; compyuta na vifaa       vya compyuta na mawasiliano.
7. Kuuza software; mfano Antivirus, Operating Systems, Pastel, Tally, Myob, n.k
8. Kushona na kuuza nguo.
9. Kufungua Duka la kuuza nguo mpya; suit, socks, batiki, nguo za asili, Mashuka, Mashati, Suruali,
10. Ufugaji wa mifugo mbalimbali mfano Kondoo, Mbuzi, Ng’ombe, Kuku, Bata, na wengine.
11. Kufungua stationery, kuuza (supply) vitabu na vifaa mbalimbali ktk mashule na vyuo.
12. Kutoa ushauri mbalimbali wa Kitaalamu.
13. Kuuza viazi, mahindi, mihogo, kutengeneza popcorn na kuziuza.
14. Kusajili namba za simu na kuuza vocha
15. Kuwa na mradi wa Pikipiki zisizotumia mafuta na zinazotumia mafuta
16. Kilimo cha mazao mbalimbali kulingana na hali ya hewa ya sehemu husika.
17. Kuuza Mitumba
18. Kusimamia miradi mbalimbali
19. Kufungua duka la kuuza mitambo mbalimbali
20. Kufungua banda la chakula na chips
21. Kukodisha turubai viti na meza
22. Kufungua Supermarket
23. Kufungua Saluni
24. Kufungua Bucha
25. Video Shooting & Editing.
26. Kufungua Internet cafe
27. Duka la kuuza matunda
28. Kufungua duka la kuuza vifaa vya simu za mkononi na landline.
29. Kufungua duka la vifaa vya ujenzi; cement, vifaa vya umeme, duka la mabati
30. Kutengeneza michoro mbalimbali ya majumba na miradi ya ICT
31. Kuchapa vitabu, bronchures, n.k
32. Kuanzisha kampuni ya ujenzi (Building contractor)
33. Kuuza Vifaa vya umeme wa nishati ya jua (solar) ,battery, inverter na vifaa vingine vya solar n.k
34. Kuuza maji kwa jumla na rejaleja.
35. Kutengeneza na kuuza Unga wa lishe bora.
36. Kukodisha Music
37. Kuanzisha Mradi wa Taxi
38. Kuanzisha mradi wa Daladala
39. Kuuza vifaa vya Kompyuta, laptops, converters, HDDs, Monitors, Softwares, CD Copiers na vifaa           vingine.
40. Kununua magenerator na kukodisha
41. Kufungua kampuni ya kutoa huduma za simu
42. Kufungua kampuni ya kutoa huduma za internet (ISP)
43. Kuuza mabati na vigae
44. Kujenga apartments
45. Kufungua Kisima cha mafuta ya taa au mafuta ya aina zote
46. Kufungua Duka la samaki
47. Kufungua Duka la nafaka
48. Kufungua Shule za Awali, Shule za Msingi, Sekondari na Vyuo.
49. Kujenga hostel
50. Kuuza vocha na ving’amuzi vya DStv, Zuku, Startimes, Easy TV, TNG, Digitech, Continental.
51. Kujenga mtambo wa kuzalisha umeme na kuuza katika viwanda na wananchi.
52. Ufundi simu
53. Kufungua Hospitali, Zahanati.
54. Maabara ya Macho, Meno
55. Kuchimba/Kuuza Madini
56. Kufungua ofisi ya kutoa huduma ya simu na fax
57. Kuuza miti na mbao
58. Kufungua Grocery, bar
59. Kufungua studio ya kupiga na kusafisha picha
60. Kucharge simu/battery
61. Duka la TV na vifaa vingine
62. Kuanzisha biashara ya kuuza vyakula katika sherehe na tamasha mbalimbali (catering).
63. Banda la kupigisha simu
64. Kuuza na kushona Uniform za shule
65. Kuanzisha duka la kuuza vitu kwa jumla.
66. Kufungua gereji za kutengeneza bajaji, pikipiki na magari
67. Kuuza vyuma, pembejeo, rake, jembe
68. Kuuza fanicha
69. Kufungua sehemu ya kuziba pancha za matairi
       ya magari na mitambo.
70. Kujenga nyumba za kulala wageni (hotel)
71. Kuagiza na kuuza vifaa vya aluminium.
72. Kuuza vioo
73. Kushona na kukodisha nguo za harusi
74. Kufungua yard kwa ajili ya kuosha magari
75. Kuuza mashine za kuchomelea (welding machine).
76. Kuuza vifaa vya kuvaa Site (boots, helmets etc)
77. Kununua mabasi kwa ajili ya kusafirisha wanafunzi
78. Kufungua studio ya kutengeneza vipindi vya redio na televisheni
79. Kuanzisha ofisi ya michezo ya televisheni (TV Games)
80. Kufungua benki
81. Kuwa na malori ya kubeba kokoto na mchanga
82. Kuuza vifaa mfano TV, CCTV Camera, n.k
83. Kuwa dalali wa vitu mbalimbali
84. Kuanzisha mradi wa kukodisha fork lift na winchi (crane)
85. Kuanzisha kiwanda cha kutengeneza viatu.
86. Kuanzisha viwanda mbalimbali
87. Duka la vifaa vya simu na gadgets mbalimbali zinazoendana na mawasiliano ya Vodacom, TTCL,          AIRTEL, TIGO, ZANTEL, n.k.
88. Kujenga Ukumbi wa kukodisha kwa sherehe, mikutano mbalimbali
89. Kununua matrekta, mitambo ya ujenzi wa barabara na kukodisha
90. Kutengeneza antenna na kuuza
91. Kufungua mradi wa Machine za kusafisha, kutoboa na kuchana mbao
92. Kufungua mradi wa kuuza vifaa vya Umeme wa kutumia upepo
93. Biashara ya kuagiza magari
94. Kufanya biashara za Jukebox
95. Kukodisha matenki ya maji
96. Kufungua duka la kuuza Asali
97. Kutengeneza Mikokoteni/ matoroli na kuikodisha
98. Kufungua Duka la vinyago, batiki
99. Kuanzisha huduma ya AIRTEL MONEY, MPESA, TIGOPESA, EZY PESA
100. Kuanzisha sehemu ya kufanyia mazoezi (Gym).
101. Kununua na kuuza vifaa vya kupima ardhi.
102. Kufungua duka la kuuza dawa (pharmacy).
103. Kufungua Kampuni ya Ulinzi
104. Kufungua kampuni ya "Clearing and fowarding"
105. Kuchezesha vikaragosi
106. Kuuza spea za bajaji, magari na pikipiki
107. Kuuza baiskeli
108. Kuuza magodoro
109. Kuuza vyombo mbalimbali kwa ajili ya matumizi ya nyumbani mfano bakuli, sahani, vikombe,                 vijiko,
110. Kuuza marumaru (limestones)
111. Kuuza kokoto
112. Kuuza mchanga
113. Kufundisha Tuisheni
114. Biashara za bima
115. Kampuni ya kusafirisha abiria kwa njia ya anga (ndege)
116. Biashara za kitalii
117. Biashara za meli na maboti.
118. Kampuni ya kuchimba visima
119. Kufungua ofisi ya wakili/mawakili wa kujitegemea
120. Kuuza mkaa
121. Kutengeneza mashine za kutengeneza tofali
122. Kampuni ya kupima ardhi
123. Kampuni ya magazeti
124. Kuchapa (printing) magazeti
125. Kuuza magazeti
126. Kuchimba mafuta
127. Kiwanda cha kutengeneza mabati
128. Kiwanda cha kutengeneza fanicha
129. Kiwanda cha kutengeneza matairi
130. Kutengeneza vitanda vya chuma
131. Kununua nyumba katika Maghorofa (Apartments) na kuzikodisha.
132. Kukodisha makapeti
133. Kupamba maharusi na kumbi za harusi/sherehe.
134. Mashine ya kusaga na kukoboa nafaka.
135. Kazi ya ususi na kusafisha kucha.
136. Kuuza Gypsum
137. Malori ya kubeba mafuta na Mizigo
138. Duka la kuuza mboga za majani
139. Duka la kuuza maua.
140. Kampuni ya kuzoa takataka
141. Kampuni ya kuuza magari
142. Kuuza viwanja
143. Uvuvi
144. Kutengeneza na kuuza nguzo za kujengea fensi
145. Uchoraji wa mabango.
146. Duka la kuuza silaha
147. Ukumbi wa kuonesha mpira
148. Biashara ya mlm (network marketing)
149. Yadi kwa ajili ya kupaki magari
150. Mradi wa trekta za kukodisha kwa ajili ya kilimo

majonzi na simanzi



Mtu mmoja aliyefahamika kwa jina la AHADI MGAYA mwenye umri kati ya 30-33 mkazi wa mtaa wa mwafute kata ya ilemi mkoani mbeya ameaga dunia baada ya kujinyonga usiku wa kuamkia leo.

Akiongea barozi wa mtaa wa mwafute JAPHETI MAHINYA  amesema kuwa yeye alipewa taarifa ya marehemu kutoweka nyumbani jana kupitia mke wake na marehemu kusema kuwa mpaka sasa chanzo cha tukio hilo hakijafahamika kwani hakuwa na mgogoro wowote.
Hata hivyo MAHINYA ametoa wito kwa wananchi kutojichukulia sheria mkononi na badala yake kama kutakuwa na tatizo au mgogoro wowote ni heri kushaulisha watu wanaokuzunguka kabla ya kuchukua hatua yoyote.
Nao majirani wa marehemu FRANCIS TAMIMU pamoja na SOPHIA wameeleza kupokea kwa mshituko tukio hilo na kutoa wito kwa wananchi wengine kutokuchukua hatua za kujinyonga kwa hupelekea maumivu makali kwa familia na jamii inayomzunguka.
Kwa upande wake kamanda wa jeshi la polisi mkoa wa mbeya MHAMED MPINGA amethibitisha kutokea kwa tukio hilo na kutoa wito kwa wananchi kutokatisha maisha yao kwa namna yoyote ile kwani huacha majonzi na simanzi kwa wanafamilia.

UJENZI WA VYOO SHULE YA MSINGI MAPAMBANO MBEYA



Wananchi wa mtaa wa mapambano kata ya iyela wametakiwa kuchangia ujenzi wa vyoo unaoendelea katika shule ya msingi mapambano ili kufanya mwendelezo wa sehemu alipoishia mdau aliyekuwa akijenga vyoo hivyo ndele mwaselela.

Hayo yameelezwa na afisa mtendaji wa mtaa wa mapambano katika kata ya iyela kizito nenalo katika mkutano wa wazazi uliofanyika katika viwanja vya shule ya msingi mapambano uliofanyika mapema hii leo.
Nenalo amesema wananchi hawanabudi kutambua kuwa afya ya mtoto inawahusu wote na hivyo wanapaswa kutoa mchango huo wa shilingi elfu tatu ili kuhakikisha kuwa ujenzi huo unakamilika.pia amewapongeza baadhi ya wananchi ambao wameonesha mwitikio mzuri katika suala hilo.
Mwenyekiti wa mtaa wa mapambano mwinjilisiti mwampetele amesema kuwa wananchi wanatakiwa kujitoa kwa vitendo na siyo maneno ikiwa ni pamoja na kuhudhuria mikutano inayoitishwa kwa lengo la kujua maendeleo ya mtaa wao.
Kwa upande wake joji mwangonele ambaye ni mwenyekiti wa kamati ya shule ya msingi mapambano amesema kuwa wazazi hawanabudi kutilia mkazo katika kufuatilia maendeleo ya watoto wao ili kuhakikisha yanakuwa mazuri.
Nao baadhi ya wazazi waliohudhuria mkutano huo Richard salingo pamoja na anastazi mwampashe wameeleza kuwa suala hilo wamelipokea vizuri na kuwataka wale ambao bado wanasitasita katika masula haya ya maendeleo kutokufanya hivyo.

nini umhimu wa mahali?

wanawake walio wengi wamekuwa wakiteseka sana katika ndoa zao na huwa wanajifikiria sababu nini lakini hawana majibu.
yafuatayo ni maswali ya nkujiuliza juu ya suala la mahali;
(a)Adamu alitoa mahali kwa nani?

(b)kama mahali ni zawadi kwa wazazi wa mtoto wa kike,je mtoto wa kiume hajalelewa na wazazi?

Jumanne, 21 Novemba 2017

JIELIMISHE UPATE KUELIMIKA

wanawake walio wengi wamekuwa wakiteseka sana katika ndoa zao na huwa wanajifikiria sababu nini lakini hawana majibu.
yafuatayo ni maswali ya nkujiuliza juu ya suala la mahali;
(a)Adamu alitoa mahali kwa nani?

(b)kama mahali ni zawadi kwa wazazi wa mtoto wa kike,je mtoto wa kiume hajalelewa na wazazi?