Jumamosi, 14 Aprili 2018

Habari kubwa za Magazeti ya TZ leo January 14 2018 Dini, Michezo na Hardnews











on
Ni asubuhi nyingine tena na habari kubwa kwenye Magazeti ya Tanzania January 14 2018 kuanzia ya, Udaku, Michezo na Hardnews kujionea yote makubwa yaliyoandikwa
EXCLUSIVE: ‘SIJAJUTA NA SITEGEMEI KUJUTA”-LOWASSA

Soma na hizi

Tupia Comments

Advertisement




DIMBWI LA MAHABA:

 Namna ya kumtambua mwenza anayekufaa



NI jambo la kawaida wengi wetu kuingia kwenye uhusiano, huku tukiwa na matumaini kwamba wenza tulio nao watakidhi vigezo vyetu na hivyo kutufaa katika maisha yetu ya uhusiano.
Hata hivyo, ndani ya uhusiano huo hukabiliwa na mtihani mkubwa wa namna ya kumtambua mwenza uliye naye kama ndiye anayekufaa kuwa naye katika maisha yako yote.
Jambo la msingi, ni kuhakikisha unapokuwa kwenye uhusiano unaweka malengo yako kwa kuhakikisha mwenza uliye naye unamfahamu vyema na si tu kuangalia yale mambo yanayokupendeza wewe tu.
Kumbuka kuwa wengi wetu tunapokuwa kwenye uhusiano siku za mwanzoni hupenda kuficha tabia zetu na uhalisia wetu na kujaribu kila njia kuhakikisha unafanya matendo yanayompendeza mwenza wako tu.
Hivyo ni vyema kutoingia kichwakichwa kutokana na ukweli kuwa mvulana mtanashati au msichana mrembo unayemuona leo anaweza kuwa si mwaminifu au asiye na maadili na huenda katika uhusiano wenu huo huko mbeleni lazima atakuletea shida.
Hapa ndiyo maana nasema ni vyema ukawa mwangalifu kwani huenda ukaona tu mambo unayotaka kuona. Hakikisha unamtambua vyema mwenza wako kiuhalisia ndipo utajua anakufaa au la.
Jaribu kupima uhusiano huo kulingana na matukio, kwa maana ya inapotokea shida, furaha, ukiwa na fedha au ukiishiwa. Hayo ni machache tu yatakuwezesha kuona ni mwenza wa aina gani uliye naye kwenye uhusiano ulionao.
Hebu angalia inapotokea kukwaruzana mwenza wako ni mtu wa aina gani, anapenda kukusikiliza au anataka asikilizwe yeye tu hoja zake? Je analipuka kwa hasira na kuanza kutukana au anatoa fursa ya kusikilizana na kushauriana?
Yapo mambo mengi yanayoweza kukuonesha aina ya mwenza uliye naye na kukurahisishia kujua kama anakufaa au la. Kumbuka kuwa si rahisi kumpata mtu asiye na matatizo jambo la muhimu ni kujifunza kuvumiliana na kuheshimiana

Jumanne, 27 Machi 2018

JESHI LA POLISI MKOA WA MBEYA LIMEKANUSHA KUTOHUSIKA NA KIFO CHA ALAIN ACHILE (22) MKAZI WA AIRPORT YA ZAMANI



Jeshi la polisi mkoa wa mbeya linawashikiria vijana kumi na wawili akiwemo kijana mmoja ambaye alifahamika kwa jina la alain achile(22) mkazi wa airpot ya zamani.
Hayo ameyasema kamanda wa wa polisi mkoa wa mbeya Mohamed mpinga wakati akizungumza na waandishi wa habari  mapema leo kuhusiana na doria zinazofanya na jeshi hilo.

Mpinga Amesema vijana hao walifanya vurugu baada ya kutokea kifo cha alain achile na kusababisha jeshi la polisi kutumia mabomu ya machozi ili kuzuia ghasia hizo.
Aidha  amesema mtuhumiwa huyu pamoja na wenzake baada ya kukamatwa walifikishwa kituo kikuu cha polisi mbeya mjini na kufunguriwa  mashitaka ya uzembe na ukorofi.

Mnamo 25.03.2018 majira ya 10.45 asubuhi mtuhumiwa alain achile alidhaminiwa na ndugu zake na kwenda nyumbani kwao na na majira ya saa 18.00 jioni walipewa taarifa ya kifo cha cha alain achile.

Ameongeza kwa kusema vijana hao walikwenda kufanya vurugu nymbani kwa mwenyekiti wa serikali ya mtaa boaz kazimoto(74)kwa kumtuhumu kuwa ndiye aliyewaita polisi kumkamata marehemu.

Halikadhalika walikwenda ofisi ya afisa mtendaji wa kata ya iyela na kubomoa milango yote,kuharibu samani na baadhi ya nyaraka na kwenda nyumbani kwa askali H.4325 PC YOHANAwa kikosi caha kutuliza ghasia na kuvunja yamadirisha ya  nyumba yake na kutoa kauli ya kuchoma nymba hiyo na kuvunja kuvunja gari ya polisi wilaya ya mbeya mjini yenye usajili PT1987 aina ya toyota.

Kamanda amewataja watuhumiwa nane waliohusika na vurugu hizo kuwa ni ELIUD DAUD(22),BARIKI MASUDI(30),ISSA NELSON(26),ROBART MWANGUPILI(24)WAKAZI WA IYELA NA FRANK KILEMI(33),KRIST NELSON(33)ESTOM MBALO(24)FELIX MBILINYI(21)WAKAIZ WA AIRPOT YA ZAMANI na upelelezi utakapo kamilika watuhumiwa watafikishwa mahakamani.
Hata Hivyo MPINGA Amekana Kuhusika Kwa Jeshi La Polisi Kuhusiana Na Kifo cha Alaini Achile Badala Yake Amefungua Jalada La Uchunguzi (PE) Kupitia Ofisi Ya  Mkuu  Waupelelezi Wa Amkosa Ya Jinai(RCO)

Jumamosi, 24 Machi 2018

WAZIRI MKUU AWATAKA VIJANA WAFANYE KAZI KWA BIDII NA MAARIFA



WAZIRI MKUU AWATAKA VIJANA WAFANYE KAZI KWA BIDII NA MAARIFA

*Asisitiza kwamba kazi ndiyo msingi wa maendeleoWAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amewataka vijana wafanye kazi kwa bidii na maarifa kwa sababu kazi ndiyo msingi wa maendeleo yao na Taifa kwa ujumla.Pia amewasihi wananchi wanaoishi katika maeneo ya mipakani wahakikishe suala la kulinda mipaka hiyo linapewa kipaumbele ili kuimarisha amani na utulivu nchini.Waziri Mkuu ametoa kauli hiyo leo (Jumamosi, Machi 24, 2018) wakati akizungumza na wananchi alipowasili katika uwanja wa ndege wa Nachingwea.Waziri Mkuu ambaye yuko wilayani Ruangwa kwa ziara ya kikazi ya siku mbili amesema ili vijana waweze kupata maendeleo lazima wafanye kazi kwa bidii.Pia Waziri Mkuu ametumia fursa hiyo kuwakumbusha wananchi wanaoishi katika maeneo ya mipakani washirikiane na Serikali katika kuimarisha ulinzi na usalama.Katika hatua nyingine, Waziri Mkuu amekagua ukarabati wa kituo cha afya cha Kata ya Mbekenyera na kuwaeleza wananchi dhamira ya Serikali ya kuwahudumia.Amesema Serikali imetoa sh. milioni 500 kwa ajili ya ujenzi wa wodi ya kujifungulia, maabara, wodi ya wanawake na wanaume na chumba cha upasuaji.“Serikali imeamua kuimarisha sekta ya afya kwa kujenga na kuboresha vituo vya afya ili kuhakikisha wananchi wanapata huduma za afya karibu na makazi yao.”Aidha, Waziri Mkuu amewataka wananchi hao waendelee kuiunga mkono Serikali yao, ambayo imedhamiria kuwatumikia ili waweze kupata maendeleo.Pia, Waziri Mkuu amekabidhi gari la kubeba wagonjwa katika kituo hicho. Gari hilo limetolewa na Rais Dkt. John Magufuli ili kuimarisha huduma za afya kituoni hapo.IMETOLEWA NA:OFISI YA WAZIRI MKUU,JUMAMOSI, MACHI 24, 2018.

Mkurugenzi SBL afanya mazungumzo na maofisa Idara ya Uhamiaji

Mkurugenzi SBL afanya mazungumzo na maofisa Idara ya Uhamiaji

Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Bia ya Serengeti (SBL) Helene Weesie, jana alifanya mazungumzo na maofisa kutoka Wizara ya Mambo ya Ndani ikiwa ni sehemu ya uboreshaji zaidi wa maslahi na mazingira ya kazi kwa wafanyakazi wa kampuni hiyo. “Tukiwa kama kampuni inayoheshimu sheria na kujali maslahi ya wafanyakazi wetu na nchi kwa ujumla, tumekuwa tukikutana na mamlaka husika ili kuhakikisha haki na maslahi ya wafanyakazi wetu yanalindwa na kuheshimiwa.,” anasema Weesie SBL imeajiri wafanyakazi zaidi ya 700 katika viwanda vyake vilivyopo Moshi, Mwanza na Dar es Salaam. Bia yake mama ya Serengeti Premium Lager ilizalishwa kwa mara ya kwanza kwa kutumia kimea kwa aslimia 100 na imeweza kushinda zaidi ya tuzo kumi za dhahabu za kitaifa na kimataifa.Tangu kuanzishwa kwake mwaka 2002, SBL imekuwa huku ikiongeza idadi ya bidhaa inazozalisha. Baada ya kisisi iikubwa cha hisa kuchukuliwa na Kampuni ya Bia ya AFRIKA Mashariki (EABL)/Diageo mwaka 2010 kumekuwepo uwekezaji mkubwa amboa umefanikisha uzalishaji w3a bidhaa zenye ubora wa kimataifa na kutengeza fursa kwa Watanzania.Moja kati ya nguzo za Diageo ambayo ni kampuni mama YA sbl ni kujenga na kuwawezesha wafanyakazi wake sehemu yoyote inapofanya kazi ikiwamo Tanzania. Kutokana na hili idadi ya wataalamu wageni imepungua kwa kiasi kikubwa kutoka zaidi ya 30 hadi sita kufikia mwezi Machi 2018 ikiwa ni chini ya asilimia 1 ya nguvu kazi katika kampuni“Tunapenda kuwahakikishia wateja wetu kuwa tutaendelea kuimarisha mahusiano na wafanyakazi wetu. Tutaendelea kukidhi mahitaji yao kwa kuwahakikishia bidhaa bora ikiwa ni sehemu muhimu kwa biashara yetu,”anasema mkurugenzi huyo.Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Bia ya Serengeti (SBL) Helene Weesie,


Nape Nnauye: Mungu Aliniokoa na Mdomo wa Bunduki ya Wanyama Wasiopenda Haki Tanzania

Nape Nnauye: Mungu Aliniokoa na Mdomo wa Bunduki ya Wanyama Wasiopenda Haki Tanzania

Mbunge wa Mtama (CCM), Nape Nnauye amezungumzia tukio la kutishiwa bastola wakati akitaka kuzungumza na waandishi wa habari nje ya Hoteli ya Protea lililotokea baada ya kuachwa katika mabadiliko madogo ya Baraza la Mawaziri.Katika ukurasa wake wa mtandao wa kijamii wa Twitter, Nape amekumbushia tukio hilo la Machi 23, 2017 na kuandika, “mwaka mmoja uliopita tarehe kama ya leo Mwenyezi Mungu aliniokoa na mdomo wa bunduki wa wanyama wasiopenda haki! Mungu mkubwa, mbegu ya haki haifi.”Katika ujumbe huo Nape aliweka picha yake ya video akizungumza na waandishi wa habari nje ya hoteli hiyo kueleza masuala mbalimbali, huku akiwataka vijana kudai haki zao bila woga.Mtu aliyemtishia bastola Nape alikuwa pamoja na wenzake wawili ambao kwa pamoja walikuwa wakimlazimisha arudi kwenye gari lake na kuondoka, lakini mbunge huyo aligoma na ndipo (mtu huyo) aliporudi nyuma na kuchomoa bastola kutoka kiunoni kisha kumtishia kabla ya kutulizwa na mwezake.Baada ya tukio hilo watu hao walitoweka eneo hilo muda mfupi baadaye.Kufuatia tukio hilo Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mwigulu Nchemba alisema mtu aliyemtishia bastola Waziri huyo wa zamani wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo hakuwa askari wa Jeshi la Polisi.Soma: Mwigulu: Aliyemtishia Nape bastola si polisiMwigulu alieleza hayo baada ya kufungua mkutano wa kazi wa mwaka wa maofisa waandamizi wa polisi, makamanda wa mikoa na wakuu wa vikosi wa Jeshi la Polisi uliofanyika mjini Dodoma.Hata hivyo, Mwigulu alikataa kueleza kwa undani kuhusu mtu huyo kwa kubainisha anatoka taasisi gani wala jina lake.
Mwaka mmoja uliopita tarehe kama ya leo Mwemyezi Mungu aliniokoa na mdomo wa bunduki wa wanyama wasiopenda haki! Mungu mkubwa, mbegu ya haki haifi! pic.twitter.com/M6PqupQQWK— Nape Moses Nnauye (@Nnauye_Nape) March 23, 2018