Jumamosi, 14 Aprili 2018

Habari kubwa za Magazeti ya TZ leo January 14 2018 Dini, Michezo na Hardnews











on
Ni asubuhi nyingine tena na habari kubwa kwenye Magazeti ya Tanzania January 14 2018 kuanzia ya, Udaku, Michezo na Hardnews kujionea yote makubwa yaliyoandikwa
EXCLUSIVE: ‘SIJAJUTA NA SITEGEMEI KUJUTA”-LOWASSA

Soma na hizi

Tupia Comments

Advertisement




DIMBWI LA MAHABA:

 Namna ya kumtambua mwenza anayekufaa



NI jambo la kawaida wengi wetu kuingia kwenye uhusiano, huku tukiwa na matumaini kwamba wenza tulio nao watakidhi vigezo vyetu na hivyo kutufaa katika maisha yetu ya uhusiano.
Hata hivyo, ndani ya uhusiano huo hukabiliwa na mtihani mkubwa wa namna ya kumtambua mwenza uliye naye kama ndiye anayekufaa kuwa naye katika maisha yako yote.
Jambo la msingi, ni kuhakikisha unapokuwa kwenye uhusiano unaweka malengo yako kwa kuhakikisha mwenza uliye naye unamfahamu vyema na si tu kuangalia yale mambo yanayokupendeza wewe tu.
Kumbuka kuwa wengi wetu tunapokuwa kwenye uhusiano siku za mwanzoni hupenda kuficha tabia zetu na uhalisia wetu na kujaribu kila njia kuhakikisha unafanya matendo yanayompendeza mwenza wako tu.
Hivyo ni vyema kutoingia kichwakichwa kutokana na ukweli kuwa mvulana mtanashati au msichana mrembo unayemuona leo anaweza kuwa si mwaminifu au asiye na maadili na huenda katika uhusiano wenu huo huko mbeleni lazima atakuletea shida.
Hapa ndiyo maana nasema ni vyema ukawa mwangalifu kwani huenda ukaona tu mambo unayotaka kuona. Hakikisha unamtambua vyema mwenza wako kiuhalisia ndipo utajua anakufaa au la.
Jaribu kupima uhusiano huo kulingana na matukio, kwa maana ya inapotokea shida, furaha, ukiwa na fedha au ukiishiwa. Hayo ni machache tu yatakuwezesha kuona ni mwenza wa aina gani uliye naye kwenye uhusiano ulionao.
Hebu angalia inapotokea kukwaruzana mwenza wako ni mtu wa aina gani, anapenda kukusikiliza au anataka asikilizwe yeye tu hoja zake? Je analipuka kwa hasira na kuanza kutukana au anatoa fursa ya kusikilizana na kushauriana?
Yapo mambo mengi yanayoweza kukuonesha aina ya mwenza uliye naye na kukurahisishia kujua kama anakufaa au la. Kumbuka kuwa si rahisi kumpata mtu asiye na matatizo jambo la muhimu ni kujifunza kuvumiliana na kuheshimiana

Jumanne, 27 Machi 2018

JESHI LA POLISI MKOA WA MBEYA LIMEKANUSHA KUTOHUSIKA NA KIFO CHA ALAIN ACHILE (22) MKAZI WA AIRPORT YA ZAMANI



Jeshi la polisi mkoa wa mbeya linawashikiria vijana kumi na wawili akiwemo kijana mmoja ambaye alifahamika kwa jina la alain achile(22) mkazi wa airpot ya zamani.
Hayo ameyasema kamanda wa wa polisi mkoa wa mbeya Mohamed mpinga wakati akizungumza na waandishi wa habari  mapema leo kuhusiana na doria zinazofanya na jeshi hilo.

Mpinga Amesema vijana hao walifanya vurugu baada ya kutokea kifo cha alain achile na kusababisha jeshi la polisi kutumia mabomu ya machozi ili kuzuia ghasia hizo.
Aidha  amesema mtuhumiwa huyu pamoja na wenzake baada ya kukamatwa walifikishwa kituo kikuu cha polisi mbeya mjini na kufunguriwa  mashitaka ya uzembe na ukorofi.

Mnamo 25.03.2018 majira ya 10.45 asubuhi mtuhumiwa alain achile alidhaminiwa na ndugu zake na kwenda nyumbani kwao na na majira ya saa 18.00 jioni walipewa taarifa ya kifo cha cha alain achile.

Ameongeza kwa kusema vijana hao walikwenda kufanya vurugu nymbani kwa mwenyekiti wa serikali ya mtaa boaz kazimoto(74)kwa kumtuhumu kuwa ndiye aliyewaita polisi kumkamata marehemu.

Halikadhalika walikwenda ofisi ya afisa mtendaji wa kata ya iyela na kubomoa milango yote,kuharibu samani na baadhi ya nyaraka na kwenda nyumbani kwa askali H.4325 PC YOHANAwa kikosi caha kutuliza ghasia na kuvunja yamadirisha ya  nyumba yake na kutoa kauli ya kuchoma nymba hiyo na kuvunja kuvunja gari ya polisi wilaya ya mbeya mjini yenye usajili PT1987 aina ya toyota.

Kamanda amewataja watuhumiwa nane waliohusika na vurugu hizo kuwa ni ELIUD DAUD(22),BARIKI MASUDI(30),ISSA NELSON(26),ROBART MWANGUPILI(24)WAKAZI WA IYELA NA FRANK KILEMI(33),KRIST NELSON(33)ESTOM MBALO(24)FELIX MBILINYI(21)WAKAIZ WA AIRPOT YA ZAMANI na upelelezi utakapo kamilika watuhumiwa watafikishwa mahakamani.
Hata Hivyo MPINGA Amekana Kuhusika Kwa Jeshi La Polisi Kuhusiana Na Kifo cha Alaini Achile Badala Yake Amefungua Jalada La Uchunguzi (PE) Kupitia Ofisi Ya  Mkuu  Waupelelezi Wa Amkosa Ya Jinai(RCO)